
Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022: Tume ya uchaguzi Kenya imebadili mpango kazi ili kuharakisha ujumlishaji wa matokeo ya kura za urais
Ikiwa ni siku ya nne sasa wakenya wakisubiri kwa hamu na ghamu kumjua rais wao mpya, Tume huru ya uchaguzi na mipaka ya Kenya IEBC imelazimika kubadili mpango wake wa kazi ilikuharakisha ujumlishaji wa matokeo ya uchaguzi wa urais mbali na kuhakiki stakabadhi zinazotoka katika maeneo yote nchini.
13 Agosto, 2022